Journalist•| Blogger•| Researcher•| Entrepreneur•| Real patriot•| Prospective husband•| Trapper changes
Tuesday, 31 March 2015
KUELEKEA KURA YA MAONI YA KATIBA PENDEKEZWA.....TUCHAMBUE PAMOJA
Kufuatia kura ya maoni ya katiba pendekezwa.
Kwa mujibu wa ratiba za serikali na taarifa
tulizonazo wananchi wa tanzania wenye umri
uliothibika kuwa na uwezo wa kupiga kura yaani
umri wa miaka 18 na kuendelea tarehe 31th
April Mwaka huu tutaenda kwenye hatua ya
kuipigia katiba pendekezwa kura ya kuikubali au
kuikataa licha ya changamoto zilizopo, ambazo ni
mkanganyiko wa hatma ya kujiandikisha kwa
wenye sifa kwa muda uliobaki wa siku chache
zijazo,Pili asilimia nyingi au wastani waoenda
kupiga kura kutokupata nakala za rasimu
pendekezwa, Tatu kwa mujibu wa sheria ya
mabadiliko ya katiba kungepaswa hadi leo ziwepo
team mbili zitakazo ratibu kampeni ya
wanayokubali na ya wanaokataa..
Tukiachana na hayo tupate kutazame katiba
pendekezwa kidogo.
kiukweli katiba pendekezwa imetazama vya
kutosha umuhimu wa haki za binadamu katika
ibara 36 Hadi Ibara Ya 59. imeainisha vyema haki
za binadamu na kuzitafsiri vema..
Katika mapungufu ya katiba hii pendekezwa
ambayo inasubiri hatua ya reforendum.
Moja: Tutazame ibara ya 124 kuhusu serikali za
mitaa. katika ibara hii kiukweli nilitegemea
ingetaja sifa za watendaji katika kila ngazi.ila
katiba pendekezwa haina sifa hizi.
Pili: Tutazame ibara ya 121 kuhusu katibu mkuu
kiongozi. Ibara hii imeainisha mamlaka ya katibu
mkuu kiongozi kuwa ni
1. Katibu wa baraza la mawaziri.
2. katibu wa usalama wa taifa.
3. mwenyekiti wa kamati maalumu ya makatibu
4. mkuu wa utumishi wa umma.
Ukitazama upatikanaji wa katibu mkuu huyu
unaleta mashaka sana kwa kuwa atatokana na
makatibu wengine ambapo ni jambo la
kustajabisha kuwa mtu huyu atawezaje kumudu
kazi zote zaidi ya makatibu wenzake?.
Nne: sifa za mbunge. rasimu ya Tume iliona
umuhimu wa wabunge wa kutunga sheria,
kuishauri na kusimamia serikali, Ikaweka kigezo
cha elimu. ila katiba pendekezwa imeweka kigezo
cha kujua kusoma na kuandika pekee huku
ikisema mawaziri watatokana na wabunge. hapa
napata maswali mengi sana. baadhi ni:-
1. endapo asilimia kubwa ya wabunge
watakaochaguliwa watakuwa wanajua kusoma na
kuandika pekee tutakuwa na mawaziri wa dizaini
hiyo hiyo?. jibu ni ndio.
2. endapo tutatungiwa sheria na watu wanaojua
kusoma na kuandika pekee nani ataiingiza katika
mfumo wa lugha ya kizungu?. sina jibu hapa.
3. endapo itakuwa ni kujua kusoma na kuandika
pekee je bajeti nani atatusaidia kupanga? hili
linakuja baada ya kupata uongozi wa serikali
(mawaziri) anaejua kusoma na kuandika pekee..
Wengi Tumezoea Kuongelea Muundo Wa
Muungano Pekee. Ila Katiba Pendekezwa Ina
Madhaifu Mengi... Haya Ni mawazo yangu kwa
katiba pendekezwa na nimepost leo kwa sheria
inaniruhusu na kukuruhusu kujadili katiba
pendekezwa pia zimebaki siku zinazotakikana
kwa sheria ya mabadiliko ya sheria...
Tuendelee Kuichambua Katiba Pendekezwa
Tuchekiane Kwenye Twitter @shadrackmafie.
Subscribe to:
Posts (Atom)