Saturday, 12 September 2015

Muigizaji ambae pia ni mbunge nchini Nigeria Desmond Elliot ameongelea hatma ya uigizaji wake


Muigizaji maarufu wa Nollywood ambaye sasa ni Mbunge, Desmond Elliot amesema kuwa kwa sasa anapumzika kufanya filamu ili ajikite vema kwenye siasa.



Amesema kuwa halitakuwa jambo la busara kuchanganya mambo ya uigizaji na maisha yake mapya ya siasa.

“Kazi ya ubunge sio rahisi, nitaonekana sio muwajibikaji kama nitaendelea kuigiza huku nina majukumu mengi ya ubunge” Desmond aliiambia Myjoyonline.

Desmond alijitosa kwenye siasa mwaka 2014 na kugombea Ubunge (Lagos State of Assembly) kwenye uchaguzi wa mwaka 2015, ambapo alishinda kupitia chama chake cha APC.

Ilani ya uchaguzi ya CCM 2015-2020

Hii hapa ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi 2015-2020. Click hapa kuidownload Ilani CCM 

Friday, 11 September 2015

Full interview ya Tommy Thomas na Evance Lyatuu.

Nimekuwekea interview  kati ya Msanii Tommy Thomas na Exelent Boy Evance Lyatuu iliyofanyika Moshi Fm katika kipindi cha Top fleva kinachofanyika kila ijumaa.
Tommy Thomas akiwa katika pozi kali.

Tommy Thomas akiwa amesimama ndani ya studio namba 2 za Moshi Fm tayari kwa interview katikati ni Shadrack Mafie na wakwanza ni Simon Salvatory wakifatilia mahojiano.

Moja kati ya mambo aliyofunguka ni kuhusu ishu kugombana na maproduser amapo amesema ni kweli amewahi kugombana na moja kati ya produser wake kwa kuwa alikuwa akizungushwa sana kwa kitendo cha kuambiwa kuwa asubiri kila akitaka kufanyiwa kazi. Akaongeza kuwa ilishafikia hatua ya kurekodi pembeni kukiwa na polisi.


Pia Tommy Thomas  anaetamba na nyimbo  yake mpya ya Twende aliyoshirikiana na Wolter Chilambo ameweka wazi wazo lake la kutoa video ya wimbo wake hivyo mashabiki wake wajiandae kupata mambo mazuri kutoka kwake.


× Mazingira aliyokulia nje ya muziki
×Amezungumziwa na ishu ya wimbo wa Roma Mkatoliki kufungiwa.
×Pia amemtaja nani anafaa kuwa raisi yote hayo yapo katika audio hii Click hapa  FULL INTERVIEW  kuisikiliza.

New Song: Tommy Thomas ft Wolter Chilambo-Twende


Nimekuwekea brand new song kutoka kwa msanii wa HIP HOP kutoka Mkoani Kilimanjaro wa kuitwa Tommy Thomas akiwa ameshirikiana na Wolter Chilambo. Wimbo unaoenda kwa jina "Twende" alifanyikia katika studio za Frezzo record mikono ya Aidan machord. click  HAPA KUDOWNLOAD  Tommy Thomas ft Wolter Chilambo-Twende.

Wednesday, 9 September 2015

New Video: Mo Music-Nitazoea



Mo Music ameamua kufuta kiu ya mashabiki wake waliokuwa wakisubiri kwa shahuku kubwa video ya single yake anayotamba nayo inayoenda kwa jina nitazoea.

Jana msanii huyo aliamua kuachia exclusive video hiyo. Kuipata unaweza kubofya HAPA KUDOWNLOAD pia unaweza kushirikisha na wengine.

Nashangazwa na Magufuli kushangazwa na mambo ya Chama chake.







Mwaka huu ni Mwaka ambao Tanzania inatarajia kuandika historia nyingine mpya ya Taifa hili ikiwa ni mwaka ambao waTanzania wataamua hatma ya nani au chama gani kitaunda serikali ya awamu ya tano tangu kupata uhuru miaka 53 iliyopita.

Chama cha Mapinduzi ambacho ni zao la TANU kimekuwa kikiaminiwa na watanzania kwa miaka mingi sana kwa utendaji wake, japo kwa siku za hivi karibuni vyama vya upinzani vimeonekana kuimarika sana kwa kujengea hoja madhaifu ya Serikali.

Nije kwenye lengo la kuchukua kalamu yangu, Dr John Pombe Magufuli ni mgombea uraisi kwa tiketi ya chama cha mapinduzi na tumemshuhudia akizunguka mikoani kunadi ilani za chama chake ambacho bado kimekamatia dola.

Katika hali isiyo ya kawaida ameonekana kushangazwa na mambo mengi ambayo yanafanywa na serikali inayoundwa na chama kilichomteua, Mavhache kati ya mengi aliyoonyesha kushangazwa nayo ni;

×Kukosekana kwa dawa katika hospitali za serikali wakati za binafsi dawa zipo.

×Mama Ntilie kuteswa na mgambo.

×Waendesha pikipiki za miguu miwili (Bodaboda) kukamatwa ovyo.

×Anashangazwa shule kukosa madawati. N.k

Naweza kumwambia hata mimi nashangazwa na yeye kushangazwa na mambo ambayo yeye anahusika kuunda serikali, yupo katika baraza la mawaziri na pia M/kiti wake wa Taifa ndie Rais wetu ambae wakiwa katika vikao vya kichama anaweza kumshauri.

Katika hali nyingine naweza kumuuliza je kama yeye aliepo ndani ya serikali ameshangazwa na kinachofanywa na serikali je sisi wananchi tujaribu kuwapa nafasi wale ambao hawajawahi kuunda serikali tuone kama wao ndio wataaacha kumshangaza???

Ni kweli changamoto haziwezi kuisha lakini kuzipunguza inafaa kupungua.Kabla wino haujaniishia naomba nimongezee mengine ya kumshangaza;

•Twiga kupanda ndege pamoja na ukubwa wote ule.

•Kushuka kwa shiligi yetu kwa poromoko kubwa sana kwa kipindi cha miaka kadhaa.

•Kupanda kwa uchumi wa taifa huku baadhi watanzania wakishindwa kumudu gharama za milo mitatu kwa siku.

•Naomba ushangazwe na mtanzania anaeweza kusema 20 million ilikuwa pesa ya mboga wakati huo kuna mwingine anaepigwa na mgambo kwa kuuza ndizi apate angalau tsh 100 ya barafu ipooze koo.

Katika yote yanayokushangaza sisi wananchi ndio tulipaswa kushangazwa nayo tukuhoji wewe ila kwa kuwa na wewe unashangazwa nayo naomba tutafute mtu atakaekuwa na majibu ya yanayokushangaza ayatatue.

Mwisho kabisa nikgusihi na nikushauri kwa dhati kabisa  kuwa tumeona vyama vinne vimeunganisha nguvu ili kupata suluhisho la yanayotushangaza na kukushangaza pia, hivyo basi kama unashangazwa kweli kutoka moyoni ungana nao ili mshangazwe wote mkiwa kitu kimoja mtafute suhuu stahiki.

Ni maoni yangu machache kwa mwenendo wa kampeni za Chama changu hadi kufikia zilipo leo. Ukiona wanasema amenunuliwa ujue ni wa muhimu ndio maana kanunuliwa.


Diamond atajwa kuwania MTV Europe Music Awards 2015 (MTV EMA)

Diamond Platnumz kwa mara nyingine amepata nafasi ya kuiwakilisha Tanzania kwenye tuzo kubwa za kimataifaa.


Ametangazwa kuwania tuzo za MTV Europe Music Awards 2015 (MTV EMA) katika kipengele cha Best African Act.


Wasanii wengine wa Afrika ambao atachuana nao kwenye kipengele hicho ni AKA (South Africa), Yemi Alade (Nigeria), Davido (Nigeria).

Hata hivyo bado anatafutwa msanii mmoja kukamilisha idadi ya nominees watano katika kipengele hicho, ambaye atapatikana kwa kura za mashabiki kupitia Twitter.

Wasanii ambao wametajwa na MTV wapigiwe kura ili apatikane mmoja ni Wizkid (Nigeria), K.O (South Africa), Stonebwoy (Ghana), Cassper Nyovest (South Africa) pamoja na Dj Arafat (Côte d’Ivoire). Kura zinapokelewa hadi September 14 saa 23:59

2015 MTV EMAs zitafanyika Octoba 25, 2015 jijini Milan, Italy ikiwa ni mara ya tatu kufanyika nchini humo na mara ya pili kufanyika kwenye jiji la Milan.

Download Nick Mbishi- Edo. (Audio)

Tumeshuhudia wasanii wengi wa bongo Movie na Bongo fleva wakijitokeza kuonyesha kumsapoti mgombea/Chama fulani cha siasa ikiwemo kwa kuwapigia kampeni majukwaani na kwa kutumia mitandao ya kijamii waliyomo.

Wamo waliojitolea kutumia vipaji vyao vya kisanaa kutoa sapoti kwa baadhi ya wagombea hao. HApa nimekuwekea wimbo wa Nicki Mbishi  aliomwimbia  mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA kwa mwavuli wa UKAWA Hm. Edward Lowassa. Click HAPA KUDOWNLOAD kusikia aliyoyasema Nick Mbishi

Tuesday, 8 September 2015

BASATA yatoa kauli baada ya kuwapo kwa minong'ono kuwa Shilole kafanya show.




Katibu Mtendaji wa baraza la sanaa la taifa (BASATA), Geofrey Mngereza ameiambia Radio 5 ya Arusha kuwa adhabu aliyopewa Shilole ya kufungiwa kutojihusisha kwenye masuala ya sanaa kwa mwaka mmoja haijafutwa.

Mngereza alidai kuwa adhabu iliyotolewa kwa Shilole imetokana na sheria na kanuni zilizotokana na bunge na kwamba kwa sasa wanakusanya ushahidi ili kuchukua hatua.

“Litachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria na kanuni zinazosema,” alisema Mngereza.

“Kwahiyo itapitia process ile ile ambayo imetumika hapo awali kuweza kutoa adhabu. Kwahiyo ni kitu ambacho kinafanyiwa kazi.”

Nimekuwekea aliyoyasema katibu mtendaji wa Nacte kuhusu mtihani wa darasa la saba.


Katibu mtendaji wa baraza la mitihani (NACTE) Dk. Charles Msonde akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar-es-salaam


Wanafunzi 775,729 walioandikishwa kufanya mtihani wa darasa la saba nchini, kesho wanaanza kufanya mtihani huo, huku idadi ya watahiniwa ikipungua ukilinganisha na walioandikishwa mwaka jana.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar-es-salaam, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk Charles Msonde amesema masomo yatakayotahiniwa kesho na kesho kutwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na Maarifa ya Jamii.

Dk Msonde amesema watahiniwa 748,514 watafanya mtihani kwa lugha ya Kiswahili na watahiniwa 27,215 watafanya mtihani huo kwa lugha ya Kiingereza ambayo wamekuwa wakiitumia kujifunzia.

“Watahiniwa wasioona walioandikishwa kufanya mitihani ni 76 na watahiniwa wenye uoni hafifu ambao wanahitaji maandishi makubwa ni 698, kati yao wavulana ni 330 na wasichana ni 368,” alisema Dk Msonde.

Amesema maandalizi ya mtihani huo yamekamilika ikiwa ni pamoja na kusambazwa kwa fomu maalumu za kujibia mtihani (OMR) na nyaraka nyingine zinazohusu mtihani huo. Alisisitiza kuwa mtihani huo unalenga kupima uelewa wa wanafunzi kwa yale waliyojifunza katika kipindi cha miaka saba.

Katibu huyo wa Necta alizitaka Kamati za Mikoa na Wilaya kuhakikisha kuwa taratibu zote za mitihani zinazingatiwa ipasavyo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa mazingira ya vituo vya mitihani yapo salama, tulivu na kuzuia mianya yote inayoweza kusababisha udanganyifu.

“Mtihani huu ni muhimu kwa Taifa kwa sababu hutumika katika uchaguzi wa wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari. Ni matarajio yetu kwamba wanafunzi wataufanya mtihani huo kwa kuzingatia taratibu zote za mtihani ili matokeo yaonyeshe uwezo wao,” alisema.

Sheria ya ndoa ya kanisa Katoliki huenda ikabadilika na kuwa hivi.


Jopo la wanasheria wa kanisa Katoliki lililoundwa mwaka jana na Papa Fransisi kwa lengo la kupitia sheria za kanisa hilo

Papa Francis anatarajia kurahisisha taratibu zinazoruhusu wafuasi wa kanisa katoliki waliooana kutoa talaka na kuolewa tena huku wakibakia kuwa wafuasi wa katika kanisa hilo .
Maelezo ya taratibu hizo yanatarajiwa kutangazwa mjini Vatcan baadaye leo .
Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa mwaka jana kupiga msasa mbinu ya kurekebisha taratibu hizo zinazoruhusu wanandoa kuachana na kupunguza gharama .

Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa mwaka jana kupiga msasa
Bila sheria hiyo wanandoa wa kikatoliki wanaotalikiana na kuolewa upya hutazamwa kama wazinifu na hawaruhusiwi kupokea komunio.

Papa Francis hatabadilisha mafunzo ya katoliki kuhusu kuachana kwa wanandoa , lakini atawezesha kurahisisha wanandoa wenye matatizo kuthibitisha kuwa ndoa yao haikuwa ya maana tangu mwanzo.

Chanzo: bbcswahili

Ulikuwa umeipata hii iliyowakuta wafuasi wa CCM kule Morogoro?? iko hapa




Watu wawili wamepoteza maisha na wengine kujeruhiwa kutokana na mkanyagano uliotokea juzi Uwanja wa Jamhuri, Morogoro katika mkutano wa kampeni za mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli.

Tayari jana, Mwenyekiti wa CCM taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete  amewatembelea majeruhi hao waliolazwa Hospitali ya Mkoa Morogoro.

Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk Ritha Lyamuya amesema walipokea watu 19 waliokuwa na majeraha yakiwemo ya kuvunjika maeneo mbalimbali ya mwili na kuongeza kuwa miongoni mwao, wawili walikufa kutokana na kuumia vibaya.

Aidha Dk Lyamuya alisema kuwa wagonjwa ambao bado wamelazwa wako 10 na wengine saba walitibiwa na kuruhusiwa.

Dk Lyamuya alisema kuwa waliokufa ni pamoja na mwanamke anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 42 na mtoto wa umri wa miaka 12 aliyejulikana kwa jina la Ramadhan Abdalah.

Uwanja wa Jamhuri juzi ulifurika watu wakati mgombea urais kwa tiketi ya CCM John Magufuli alipokwenda kwa ajili ya kufanya kampeni.

Mara tu baada ya Magufuli na viongozi wengine kuondoka uwanjani hapo, ndipo hali ya kusukumana na kukanyagana ilitokea getini wakati watu wakitoka.

Full story kuhusu ziara ya Lowassa jana jijini Dar





Mgombea urais wa Chadema anayeungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa amesema hakutakuwa na muda wa kupoteza iwapo atachaguliwa akisema ataanza kushughulikia ahadi zote ikiwamo ya ujenzi wa viwanda kwa ajili ya kutatua tatizo la ajira mara tu baada ya kuapishwa.

Akizungumza kwenye mikutano ya hadhara, Bunju na baadaye Mbezi mkoani Dar es Salaam, Lowassa alisema kila alichoahidi ataanza kukifanyia kazi punde tu baada ya kuapishwa: “Nitajenga viwanda kukabiliana na ajira, ada za shule na mengine ndani ya siku hizo.

“Nikiingia madarakani, hakuna mgeni atakayefanya biashara bila kuingia ubia na wazawa. Lazima tuwajali vijana wetu kwa kuwajengea mazingira wezeshi,” alisema mgombea huyo aliyewasili Bunju saa 9.30 alasiri akitokea Tabora.

Ili kufanikisha hayo, aliwataka vijana kulinda kura zao siku ya uchaguzi ili zisiibwe.

Akizungumza katika mkutano wake uliofanyika kwenye Uwanja cha Shule ya Msingi Bunju ‘A’, Lowassa alisema wananchi wana wasiwasi na NEC kwamba haitatenda haki kwa sababu ya ukaribu wake na CCM.

Aliwataka vijana kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi na kufanya kazi mbili, kwanza kupiga kura na pili ni kulinda kura zao huku akisisitiza kwamba ana uhakika kwamba hataibiwa kura ng’o.

Aliwataka wananchi kufanya uamuzi mgumu kuiondoa CCM madarakani ili wajihakikishie huduma bora za jamii katika serikali ya awamu ya tano.

Alisema zimebaki siku 48 kwa wananchi kuamua hatima ya maisha yao yajayo akiwataka kuwachagua wagombea wa Ukawa ili waondoe msongamano wa magari jijini, kuboresha mfumo wa elimu kuanzisha viwanda vitakavyotengeneza ajira kwa wananchi.

Awali, akimkaribisha Lowassa, Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye alisema ili kuepuka vurugu, lazima CCM wakubali kushindwa na kupisha serikali mpya ya Ukawa.

Alisisitiza kuwa ameihama CCM baada ya kubaini kuwa mabadiliko hayawezi kupatikana ndani ya chama hicho.

Alimtaka mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Magufuli kuzungumzia kashfa mbalimbali zinazoikabili Serikali ya sasa ambazo ni pamoja na usafirishwaji wa twiga, dawa za kulevya na pembe za ndovu.

“Ndani ya CCM huwezi kufanya chochote, CCM ni shida,” alisema Sumaye na kuongeza kuwa uchumi umeshuka tofauti na miaka 10 iliyopita.

Alisema Ukawa ikiingia madarakani, itahakikisha fedha zote zilizofichwa nje ya nchi zinarudishwa na wahusika wake kuchukuliwa hatua za kisheria.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema: “NEC watasababisha machafuko kwa kuibeba CCM. Chama hicho kwa sasa hakibebeki, sasa wameanza kuwatumia watu kumchafua Lowassa.”

Alisema ziara ya kampeni za umoja huo katika mikoa saba, imeonyesha kwamba wananchi wako tayari kwa mabadiliko na kuipokea serikali ya Ukawa.

Awali, mgombea ubunge wa Jimbo la Kawe (Chadema), Halima Mdee alimtaka Lowassa kusaidia kutatua migogoro ya ardhi katika jimbo hilo hasa eneo la Boko.

Alisema uhakiki wa majina katika daftari la kudumu linaendeshwa kihuni kwa sababu wananchi wakienda kwenye vituo hawalioni.

Mgombea huyo wa urais alihitimisha kampeni zake Bunju saa 10.30 jioni na kuelekea Mbezi kwa ajili ya mkutano mwingine ambao ulimalizika saa 12.15 jioni.

Akiwa Mbozi

Baada ya kuwasili Mbezi saa 11.15, Lowassa aliwaomba wakazi wa Jimbo la Kibamba wamchague pamoja na mbunge na madiwani wa Ukawa ili waweze kumsaidia kuleta mabadiliko yatakayoboresha maisha ya wananchi.

Alisema kumekuwa na tuhuma nyingi dhidi yake, lakini akasema ataendelea kufanya kampeni za kistaarabu ili kuwaeleza wananchi nini anataka kukifanya.

“Wananikashifu kwa maneno mengi, eti wanashangaa mimi kupanda daladala sasa, lakini hawashangai twiga kupanda ndege,” alisema.

Awali, Sumaye alisema hawezi kujibizana na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba kwa sababu na ataonekana amepungukiwa.

Sumaye alisema Chadema ikishinda uchaguzi, kazi ya kwanza itakuwa kutaifisha na kurudisha fedha zilizowekwa na vigogo wa serikali nje ya nchi.

“Kazi ya kwanza itakuwa kurudisha fedha zilizoibwa na vigogo wa Serikali ya CCM, tutazirudisha na kuziweka katika Haz“Kazi ya kwanza itakuwa kurudisha fedha zilizoibwa na vigogo wa Serikali ya CCM, tutazirudisha na kuziweka katika Hazina yetu,” alisema.

Sumaye ambaye mara kwa mara alitumia kaulimbiu ya “CCM” na wananchi kumjibu ni “shidaaa”, alisema tangu Lowassa ajiuzulu kashfa za ufisadi wa fedha za Serikali umeongezeka.

Mbowe ambaye pia Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa, aliwataka wananchi hao kuhakikisha wanatunza vitambulisho vya kupigia kura ili waweze kufanya uamuzi sahihi Oktoba 25.

“Mlivyohamasika mnaonyesha kwamba mmekubali mabadiliko, hivyo jambo la msingi ni kutunza vitambulisho vyenu ili siku ya uchaguzi muweze kuwachagua viongozi wa Ukawa,” alisema.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kibamba (Chadema), John Mnyika aliomba kura kwa wagombea wote wa Ukawa ili waweze kuleta maendeleo.

“Umati huu unaonyesha kwamba wananchi mna imani na viongozi wanaogombea kupitia Ukawa, tunaomba mtuchague,” alisema.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ubungo kupitia chama hicho, Saed Kubenea aliwaomba wananchi wawachague viongozi wa Ukawa ili waende bungeni kuwatetea wananchi

Ilivyokuwa

Wafuasi wa Ukawa walianza kufika katika Uwanja wa Bunju A tangu saa nne asubuhi wakiwa wamejipamba kwa mavazi ya sare za vyama vinavyounda umoja huo.

Baadhi ya wafuasi hao wakiwa na bendera za vyama vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi, muda wote walikuwa wakiimba na kucheza nyimbo za Chadema.

Wafuasi hao walikuwa wakipuliza matarumbeta kwenye barabara inayopita jirani na uwanja huo huku baadhi ya magari yaliyokuwa yakipita eneo hilo, yakiunga mkono kwa kupuliza honi.

Madereva wengi kati ya hao, walikuwa wakinyanyua mikono juu na kuonyesha alama ya vidole viwili ambayo inatumiwa na Chadema.

Wafuasi wa chama hicho walipouona msafara wa Lowassa ukiwasili katika viwanja hivyo saa 9.30 alasiri walishangilia kwa sauti ya juu huku wakiimba rais, rais, rais.

Baada ya mkutano kumalizika kwenye viwanja hivyo na msafara wake kuanza safari ya kuelekea Mbezi, saa 10.40 jioni, karibu kila eneo alikopita, wananchi walionekana wakiwa wamejipanga kando ya barabara wakimshangilia, wengi wao wakionyesha alama ya vidole viwili.

Mbali ya kujipanga barabarani, katika baadhi ya maeneo, wananchi walipanda juu ya miti ili wapate kuuangalia vyema msafara huo ulipitia Goba hadi Mbezi.

Huko Mbezi, wananchi walikuwa wamefurika kwenye uwanja wa mkutano tangu saa nane mchana.

Sababu za kuchelewa


Akizungumzia sababu ya kuchelewa kwa mikutano hiyo ambao wa Bunju ulipangwa kuanza saa nne asubuhi na Mbezi saa tisa alasiri, Mbowe alisema hiyo ilisababishwa na kuunganisha safari jana hiyohiyo kutoka Tabora kupitia Dodoma.

“Tunawaomba radhi kwa kuchelewa kuanza kwa sababu ya safari ndefu,” alisema Mbowe.

Pamoja na mkutano huo kumalizika dakika 15 zaidi ya muda uliowekwa na NEC, Polisi waliokuwapo hawakuonekana kuchukua hatua yoyote.

Monday, 7 September 2015

Jambo Squad wapiga hatua nyingine


Wasanii wa kundi la Jambo Squad kutoka Arusha wamethibitisha kauli ya kuwa muziki unalipa baada ya kufungua mgahawa jijini humo.





Jambo Squad wamedai kuwa licha ya kuonekana wanafanya muziki wa tofauti, wameweza kupiga hatua kimaisha.

“Sisi ni watoto wa uswahilini, tumelelewa uswahilini so maisha tunayajua,” waliiambia XXL ya Clouds FM.

“Sisi ni watu wa biashara sio kukaakaa tu. Ila kwa sasa hivi tumeamua tuanzishe sehemu ambayo itatukutanisha na watu wetu ambayo ni Café. Ni biashara ambayo itaingiza pesa kila siku, ndio tukaamua kufungua Cafe. Ipo maeneo ya Sakina, ambapo ni karibu na Jambo Squad Camp.”

Wamedai kuwa mgahawahi huo umewagharimu fedha nyingi kuuanzisha, hali ambayo inadhiirisha muziki wa kitanzania unalipa tofauti na wengi walivyoamini nyakati za nyuma. 

Sunday, 6 September 2015