Wednesday, 22 July 2015

Ndesamburo asalimu amri

Aliekuwa mbunge wa jimbo la Moshi Mjini ndg. Felemoni Ndesamburo ameamua kuachia jimbo kwa mtu mwingine. Ni baada ya kutojitokeza kwa kuchukuwa fomu. Waliochukuwa ni hawa.


Makada watatu wa Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Wilayani moshi wamejitokeza kuomba ridhaa ya chama kuteuliwa kukiwakilisha katika ngazi ya ubunge katika jimbo la Moshi mjini.

Katibu wa chadema manispaa ya Moshi ndg. Steven LubelwaAkizungumza amesema waliochukua na kurejesha fomu kwa wakati ni...

 Eliakunda George,
 Basil Lemul Lema,
 Raphael Japhary Michael.
Pia ndg. Lubelwa alitaharifu chombo hiki kuwa tarehe ya mwisho ya kuchukua na kurejesha fomu za ubunge ndani ya chama hicho ilikuwa ni tar 19july hivyo kwa sasa ni kura za maoni zinatarajiwa kufanyika.

Mwana habari alipotaka kujua utaratibu wa kumpata mwakilishi mmoja utakuwaje Katibu Steven Lubelwa alisema Mchakato utahusisha wajumbe kutoka katika kata zote katika jimbo la Moshi Mjini huku akisema mchakato huo utafanyika katika ukumbi wa Uhuru hostel tar 23 siku ya halhamisi.



Kwa matangazo yoyote mnakaribishwa kutangaza nasi kwa bei nafuu. Kwa mawasiliano wasiliana nasi kwa simu +255766442555, au email shadrackmafie@yahoo.com

Sunday, 19 July 2015

Sekeseke la uchaguzi ngazi ya ubunge jimbo la Moshi mjini.

Kuelekea uchaguzi mkuu, wimbi la watangaza nia wanaosaka kupokea bakora la aliekuwa Mbunge wa Moshi mjini Mh. Felemon Ndesamburo linaendelea kuchukuwa sura mpya. Hawa ni baadhi ya wanaolitamani kwa upande wa Chama cha mapinduzi.
 Kada wa chama cha mapinduzi Manispaa ya Moshi Daudi Mrindoko akiwa ameambatana na mkewe katika ofisi za CCM wilaya ya Moshi kuchukuwa Fomu ya kuwania ubunge kwa tiketi ya Chama cha mapinduzi.



Kada mwingine na mtangaza nia ndg. Priscus Tarimo akikabidhiwa fomu ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya Chama cha mapinduzi katika nafasi ya ubunge katika jimbo la Moshi mjini. 


Priscus akitoa maelezo binafsi kwa katibu msaidizi wa CCM wa wilaya ya Moshi. Mh Donatha Mushi.

Mtia nia mwingine ambae ni mwakilishi wa jamii ya Bantu Unioni Bwana Omary Mwaliko akirejesha fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha mapinduzi kumpitisha kukipeperushia bendera katika ngazi ya ubunge jimbo la Moshi mjini, uchaguzi ujao.


EDmund Rutaraka ambae ni naibu kamanda wa vijana CCM Akipokea fomu ya kuomba ridhaa ya chama chake.

Ikumbukwe kwa mujibu wa ratiba ya Chama cha mapinduzi mwisho wa kuchukuwa na kurudisha fomu ni Jumapili ya tarehe 19 July2015.


Picha na Dixon Busagaga.

Ungana nami kwa matukio yote yanayojiri.

Piga *149*01#kufurahia huduma bomba za vodacom.