Wednesday, 22 July 2015

Ndesamburo asalimu amri

Aliekuwa mbunge wa jimbo la Moshi Mjini ndg. Felemoni Ndesamburo ameamua kuachia jimbo kwa mtu mwingine. Ni baada ya kutojitokeza kwa kuchukuwa fomu. Waliochukuwa ni hawa.


Makada watatu wa Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Wilayani moshi wamejitokeza kuomba ridhaa ya chama kuteuliwa kukiwakilisha katika ngazi ya ubunge katika jimbo la Moshi mjini.

Katibu wa chadema manispaa ya Moshi ndg. Steven LubelwaAkizungumza amesema waliochukua na kurejesha fomu kwa wakati ni...

 Eliakunda George,
 Basil Lemul Lema,
 Raphael Japhary Michael.
Pia ndg. Lubelwa alitaharifu chombo hiki kuwa tarehe ya mwisho ya kuchukua na kurejesha fomu za ubunge ndani ya chama hicho ilikuwa ni tar 19july hivyo kwa sasa ni kura za maoni zinatarajiwa kufanyika.

Mwana habari alipotaka kujua utaratibu wa kumpata mwakilishi mmoja utakuwaje Katibu Steven Lubelwa alisema Mchakato utahusisha wajumbe kutoka katika kata zote katika jimbo la Moshi Mjini huku akisema mchakato huo utafanyika katika ukumbi wa Uhuru hostel tar 23 siku ya halhamisi.



Kwa matangazo yoyote mnakaribishwa kutangaza nasi kwa bei nafuu. Kwa mawasiliano wasiliana nasi kwa simu +255766442555, au email shadrackmafie@yahoo.com

No comments:

Post a Comment