Journalist•| Blogger•| Researcher•| Entrepreneur•| Real patriot•| Prospective husband•| Trapper changes
Wednesday, 18 March 2015
NAPE AZICHAPA NA M/KITI...ARUSHA
Nape Nnauye amemfanyia
vurugu kubwa Onesmo Nangole Mwenyekiti wa
CCM Mkoa wa Arusha kwa sababu ya chuki za
kisiasa tu
Umri wa Nape na Nangole haulingani lakini
jambo la ajabu Nape anampa maelekezo kwa
njia ambayo inaonyesha alidhamiria
kumdhalilisha kwa kuwa Nangole anahusishwa
na kambi ya Lowassa
Nape alianza kumtuhumu Nangole kuwa
ameandaa mapokezi hafifu kwa ujumbe wa
Sekretarieti ya chama taifa na pia kukiuka
itifaki muda wote hasa ziara ya Monduli na
Karatu kwa sababu ya njaa njaa zake. Jambo
hili liliwakera wengi na hasa baadhi ya makada
kutoka UVCCM na Umoja wa wanawake huku
Nangole akimwambia Nape awe na nidhamu
angalao kwa umri wake kwa kuwa chama hicho
wamekipigania na hakuna mwenye hatimiliki
Mzee Justine Kaaya aliingilia kati na kuwaambia
aibu hii inapaswa kumalizwa kwa kuwa eneo
hilo watu walikua wakipita na kumtaka Nape
kuomba radhi kitendo kilichomkasirisha na
kujibu kuwa hawezi kuwaomba radhi vibaraka
wa watu bali anasimamia heshima ya chama na
sio kutishwa na mafisadi na vibaraka wao
Ndipo Mwenyekiti wa Mkoa Nangole alipomjibu
akajifunze siasa kwanza maana hajawahi
kushinda uchaguzi wowote zaidi ya kubebwa na
pia ni msaliti mkubwa mwanzilishi wa chama
na kubeba mikoba ya akiba Renatus Kyabo
Ghafla Nape akamrushia ngumi Nangole na
kusababisha vurugu kubwa na kumvunjia
Miwani Mama Martina Gurtu aliyejaribu
kuingilia ugomvi huo huku Nangole akichaniwa
Shati Lake
Vijana waliokua pale Naura Spring waliingilia
kati na kuwatenganisha. Kikao cha ndani ndio
kinafanyika jioni hii kikiongozwa na Kinana ili
kumaliza swala hili.
Chanzo: JamiiForums
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment