Friday, 17 July 2015

#Arusha: Mradi wa ujenzi wa kituo cha kupima hali ya hewa umeaza kutekelezwa katika wilaya ya Meru.

Bodi ya maji ya bonde la mto pangani yenye ofisi zake wilayani Moshi,Imeanza kutekeleza  mradi wa ujenzi wa  kituo cha hali ya hewa katika wilaya ya Meru

Akizungumza na  Shadrack Mafie mhaidrolojia wa bodi hiyo ndg. Bakari Mohamed Bamba amesema kulingana na jeografia wamelazimika kujenga kituo hicho katika kijiji cha Mareu,kata ya King'ori wilayani humo.kadhalika alisema kituo hicho kitatumika kupima kuongezeka na kupungua kwa maji katika Mito.

Pia ndg Bakari aliongeza kwa kuainisha lengo la mradi kuwa ni kuwasaidia wananchi na wakaazi waishio mabondeni kwa kuwa historia inaonyesha mvua nyingi zinazonyesha katika maeneo ya ukanda wa juu ndizo zinazosababisha madhara katika maeneo ya  Makiba,Malula na maeneo mengine ya ukanda wa chini.

Bwana Bakari pia alimaliza kwa kuwasihi wote watakaonufaika na mradi watumie vyema taarifa zitakazotolewa na kituo


Ungana nami√√√√



No comments:

Post a Comment