Journalist•| Blogger•| Researcher•| Entrepreneur•| Real patriot•| Prospective husband•| Trapper changes
Wednesday, 4 February 2015
MASAHA KABLA YA UCHAGUZI MKUU 2015
Ni Mwiaka 53 Tukiwa Tunaongozwa Na Serikali
Inayoundwa Na Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Katika Awamu Nne, Awamu Ya Kwanza
Tuliongozwa Na Hayati Mwl Julias Kambarage
Nyerere Awamu Hii Ya Kwanza Ilikuwa Ya
Kusifika. Awamu Ya Pili Tukawa Na Mh
Mwinyi Mzee Wa Ruksa.
Awamu Ya Tatu Mh
Benjamin Mkapa Ambae Alisifika Kwa
Kuimarisha Uchumi, Japo Wananchi Walianza
Kupoteza Imani Na Chama. Na Katika Awamu
Hii Tuliyonayo Tupo Na Mh Jakaya Kikwete
Ambae Amepata Changamoto Nyingi
Zilizowafanya Wengi Kukata Tamaa Na Chama
Hiki Kilichoridhi Damu Ya TANU Iliyotutafutia
Uhuru Kutoka Kwa jkkWakoloni.
Ni Nafasi Yetu Kutafakari Ni Uongozi Upi
Unatufaa.
ANGALIZO KWA VYAMA.
1.Kutokana Na Wananchi Wa Tanzania
Kuelimika Na Kuwa Wachunguzi Wa Hali Ya
Juu Yapasa Chama Kijipange Kwa Sera
Zinazotekelezeka.
2. Chama Chochote Cha Siasa Kumwandaa
Mgombea Anaetarajiwa Na Wengi Na
Kuungwa Mkono Ili Kuweza Kupata Ushindi
Usio Na Doa.
3. Chama Chochote Kiandae Na Kufanya
Kampeni Zake Kistaharabu Pasipo Kuingiliana
Kwa Namna Yoyote Ile Itakayosababisha
Uvunjifu Wa Amani.
4. Chama Chochote Kihakikishe Wapiga Kura
Wanapata Haki Ya Msingi Ya Kujiandikisha
Kwa Kutoa Elimu Zaidi.( Kwa Kuzingatia
Tutakuwa Na Mfumo Mpya Wa BVR).
5. Chama Chochote Kielewe Kinaongea Na
Watanzania Wasomi Ambao Wanahoji Kila
Herufi Itokayo Mdomoni Kwa Mgombea Au
Kiongozi. Hapa Namaanisha Kuongea Pasipo
Kuropoka.
6. Chama Chochote Kiwe Tayari Kujibu
Maswali Magumu Yatakayojitokeza Popote
Kukiusu,Ikiwemo Kwenye Mitandao Ya
Kijamii. Hii Itakisaidia Kuaminiwa.
7. Chama Chochote Kiwe Na Utoaji Wa Elimu
Maalumu Ya Kuheshimu Na Kutii Sheria.Pia
Walitake Jeshi la Polisi Kufanya Kazi Katika
Taratibu Na Sheria.
8. Chama Chochote Kikiona Makosa Popote
Kitoe Msahada Ili Kuweza Kupatia Ufumbuzi
Ambao Utafanya Kila Kitu Kiwe Sawa Kama
Kilivopangwa.
9. Chama Chochote Kijitaidi Kutumia Lugha
Inayoeleweka Katika Utoaji Wa Sera Ili Kundi
Kubwa Liweze Kuelewa Na Kuzichambua.
Kitendo Hiki Kitafanya Kila Mtu Ajue Anapigia
Nini Au Nani Na Kwa Sababu Gani.
10. Ni Vema Na Sisi Raia Tukawa Watulivu
Katika Kuitafuta Tanzania Iliyo Bora
Itakayokua Mfano Wa Kuigwa Katika Nyanja
Zote. Uchumi Imara, Siasa Bora, Ulinzi Na
Usalama Ulioimarika NK
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment