Saturday, 12 September 2015

Muigizaji ambae pia ni mbunge nchini Nigeria Desmond Elliot ameongelea hatma ya uigizaji wake


Muigizaji maarufu wa Nollywood ambaye sasa ni Mbunge, Desmond Elliot amesema kuwa kwa sasa anapumzika kufanya filamu ili ajikite vema kwenye siasa.



Amesema kuwa halitakuwa jambo la busara kuchanganya mambo ya uigizaji na maisha yake mapya ya siasa.

“Kazi ya ubunge sio rahisi, nitaonekana sio muwajibikaji kama nitaendelea kuigiza huku nina majukumu mengi ya ubunge” Desmond aliiambia Myjoyonline.

Desmond alijitosa kwenye siasa mwaka 2014 na kugombea Ubunge (Lagos State of Assembly) kwenye uchaguzi wa mwaka 2015, ambapo alishinda kupitia chama chake cha APC.

No comments:

Post a Comment