Tuesday, 8 September 2015

Sheria ya ndoa ya kanisa Katoliki huenda ikabadilika na kuwa hivi.


Jopo la wanasheria wa kanisa Katoliki lililoundwa mwaka jana na Papa Fransisi kwa lengo la kupitia sheria za kanisa hilo

Papa Francis anatarajia kurahisisha taratibu zinazoruhusu wafuasi wa kanisa katoliki waliooana kutoa talaka na kuolewa tena huku wakibakia kuwa wafuasi wa katika kanisa hilo .
Maelezo ya taratibu hizo yanatarajiwa kutangazwa mjini Vatcan baadaye leo .
Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa mwaka jana kupiga msasa mbinu ya kurekebisha taratibu hizo zinazoruhusu wanandoa kuachana na kupunguza gharama .

Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa mwaka jana kupiga msasa
Bila sheria hiyo wanandoa wa kikatoliki wanaotalikiana na kuolewa upya hutazamwa kama wazinifu na hawaruhusiwi kupokea komunio.

Papa Francis hatabadilisha mafunzo ya katoliki kuhusu kuachana kwa wanandoa , lakini atawezesha kurahisisha wanandoa wenye matatizo kuthibitisha kuwa ndoa yao haikuwa ya maana tangu mwanzo.

Chanzo: bbcswahili

1 comment: